Mkutano wa ndani baina ya Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Rais Jakaya Kikwete na wabunge wa chama hicho uliofanyika Jumapili iliyopita mjini Dodoma, ni kama umeamsha upya makundi ya kuwania urais wa 2015, Mwananchi limebaini.
Kutokana na hali hiyo, jana chama hicho 
kililazimika kutumia nguvu kubwa kudhibiti taarifa zinazohusu kauli 
iliyodaiwa kuwa ilitolewa na Rais Kikwete, kwamba “Wanaoutaka urais 
kupitia CCM waanze kujipitisha ilimradi wasiwagawe wanachama kwa misingi
 ya makundi.”
Taarifa kuhusu ruksa hiyo inayodaiwa kutolewa na 
Rais, ndizo zilizotikisa vichwa vya habari katika magazeti ya juzi na 
jana lakini Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Nape Nnauye anasema siyo
 za kweli na kwamba Rais alilishwa maneno.
Nape jana katika mkutano na Waandishi wa Habari 
jijini Dar es Salaam alisema: “Wamemlisha maneno mwenyekiti 
wetu...inaelekea kuna kikundi cha watu wana mgombea wao wa kuchonga 
ambaye bila shaka anapungukiwa na sifa, hivyo wanajaribu kumwongezea 
sifa kwa kumlisha mwenyekiti maneno na kuwapa baadhi ya waandishi, uhuni
 huo haukubaliki.”
Wakati Nape akitoa kauli hiyo, Waziri wa Nchi, 
Ofisi ya Rais (Uhusiano na Uratibu), Steven Wassira akizungumza bungeni 
jana pia alisema taarifa kuhusu mkutano wa Rais Kikwete na wabunge 
zilipotoshwa, huku akitaka suala hilo lifafanuliwe na watendaji wa CCM.
JK na wabunge
Nape alisisitiza katika mkutano huo Rais Kikwete 
alisema ni marufuku kwa mwanachama anayetaka kugombea kwenye uchaguzi wa
 dola kujipitishapitisha na kufanya kampeni kabla ya wakati.
Habari kutoka ndani ya mkutano huo zinasema 
chimbuko la hoja ya watu wanaotaka kujinadi kwa ajili ya uongozi 
iliibuliwa na Mbunge wa Same Mashariki, Anna Killango Malecela na Mbunge
 wa Lupa, Victor Mwambalaswa ambao walihoji juu vikao vinavyofanywa na 
watu wanaosaka urais kupitia CCM kwa kuwashirikisha watendaji wa chama 
na Serikali.
Majibu ya Kikwete
Baadhi ya wabunge wameliambia gazeti hili kuwa 
Rais Kikwete katika mkutano huo alieleza kusikitishwa na kampeni za 
urais ambazo alisema zinakigawa chama.
“Sisi tunashangazwa na taarifa ambazo magazeti 
mmeziandika, ukweli ni kwamba mheshimiwa Rais alituasa kwamba tusikigawe
 chama na kwamba asingependa tuwe na mgombea mwenye makovu ifikapo 
2015,” alisema mmoja wa wabunge.
Vyanzo vyetu hivyo vilimnukuu Rais Kikwete 
akisema: “Mnaumizanaa wee, sasa inaweza kufika hiyo 2015 tutajikuta 
tukiwa na wagombea wenye plasta, sasa ikifikia hapo sijui tutaanza 
kumuuza mgombea wetu au kutibu majereha kwanza?”
Chanzo: Mwananchi.
Chanzo: Mwananchi.


 
 
 
 
 
 
 
 I’m a Freelance Web Designer & Developer. I’m an enthusiastic, creative designer and geek with 3 years of strong commercial experience and a passion for creating beautiful, accessible websites using Web Standards
I’m a Freelance Web Designer & Developer. I’m an enthusiastic, creative designer and geek with 3 years of strong commercial experience and a passion for creating beautiful, accessible websites using Web Standards
No comments:
Post a Comment
Tuachie Ujumbe wako hapa .