| +aliesimama+Mhandisi+Boniface+Muhegi+akitoa+taarifa+kwa+waziri+wa+Ujenzi+Magufu.jpg) | 
| Msajili wa Bodi hiyo, Mhandisi Boniface Muhegi aliyesimama | 
Msajili wa Bodi hiyo, Mhandisi Boniface Muhegi  alitoa wito huo jana alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari juu ya  maandalizi ya mkutano huo aliosema utaangalia kwa undani mafanikio na  changamoto katika sekta ya ujenzi nchini kwa miaka 15 tangu kuanzishwa  kwa bodi hiyo. Alisema mkutano huo utakuwa na manufaa kwao ikiwamo  kusaidia kuwapandisha madaraja na kupata alama katika maendeleo ya fani  yao huku washiriki kutoka nchi za Kenya, Uganda na Rwanda wakialikwa  kubadilishana uzoefu na washiriki wa ndani.
“Tunahamasisha ushiriki wa wakandarasi toka sekta binafsi na umma,” alisema Muhegi.
Alidokeza kuwa sekta ya ujenzi Tanzania imepiga  hatua kubwa toka kuanzishwa kwa bodi hiyo ambapo sasa ina makandarasi  7000 ikilinganishwa na 1000 waliokuwapo miaka 15 iliyopita.Mengine ni  kuongezeka kwa ubora na wingi wa kazi za ukandarasi wa ujenzi akitolea  mfano ongezeko la minara ya mawasiliano ya simu za mkononi ambayo  imetapakaa karibu nchi nzima, barabara na majengo ya k isasa.
Katika mkutano huo,mada nne zitawasilishwa kutoka  kwa wadau mbalimbali zote zikilenga changamoto na mafanikio katika sekta  ya ujenzi Tanzania ndani ya miaka15.

 
 
 
 
 
 
 
 I’m a Freelance Web Designer & Developer. I’m an enthusiastic, creative designer and geek with 3 years of strong commercial experience and a passion for creating beautiful, accessible websites using Web Standards
I’m a Freelance Web Designer & Developer. I’m an enthusiastic, creative designer and geek with 3 years of strong commercial experience and a passion for creating beautiful, accessible websites using Web Standards
No comments:
Post a Comment
Tuachie Ujumbe wako hapa .