Matangazo ya AFCON katika tv yazua mgogoro
Tuesday, January 22, 2013
MALALAMIKO yameanza kujitokeza katika maandalizi yanayoendelea ya michuano ya klabu bingwa Afrika (Afcon) itakayofanyika nchini Afrika Kusini, ambako tayari timu za mataifa yanayoshiriki michuano zimekwishaweka kambi.
Tayari Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Utangazaji nchini Nigeria (BON), Alhaji Abubakar Jijiwa, amelalamikia utozaji mkubwa wa hatimiliki kwa chombo cha habari kinachotaka kurusha matangazo hayo ya soka.
Taarifa zinaeleza ya kuwa malalamiko hayo yanajitokeza katika wakati ambao michuano ikiwa imefadhiliwa kwa karibu kila nyanja na wafadhili wakubwa
Ni kutokana na ufadhili huo Jijiwa anahoji, kama michuano imefadhiliwa kwa kiasi hicho ni kwa nini wao watozwe fedha nyingi?
Na kwa hiyo anasema; "Mashirika ya utangazaji Nigeria tumekataa kulipa Euro milioni nane kwa ajili ya haki ya chombo cha habari kurusha matangazo hayo, tunasikitika kwa Wanigeria kutoweza kuangalia matangazo haya kama walivyotaraji."
Subscribe to:
Post Comments (Atom)

 
 
 
 
 
 
 
 I’m a Freelance Web Designer & Developer. I’m an enthusiastic, creative designer and geek with 3 years of strong commercial experience and a passion for creating beautiful, accessible websites using Web Standards
I’m a Freelance Web Designer & Developer. I’m an enthusiastic, creative designer and geek with 3 years of strong commercial experience and a passion for creating beautiful, accessible websites using Web Standards
No comments:
Post a Comment
Tuachie Ujumbe wako hapa .