Matangazo ya AFCON katika tv yazua mgogoro

Tuesday, January 22, 2013

MALALAMIKO yameanza kujitokeza katika maandalizi yanayoendelea ya michuano ya klabu bingwa Afrika (Afcon) itakayofanyika nchini Afrika Kusini, ambako tayari timu za mataifa yanayoshiriki michuano zimekwishaweka kambi. Tayari Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Utangazaji nchini Nigeria (BON), Alhaji Abubakar Jijiwa, amelalamikia utozaji mkubwa wa hatimiliki kwa chombo cha habari kinachotaka kurusha matangazo hayo ya soka. Taarifa zinaeleza ya kuwa malalamiko hayo yanajitokeza katika wakati ambao michuano ikiwa imefadhiliwa kwa karibu kila nyanja na wafadhili wakubwa Ni kutokana na ufadhili huo Jijiwa anahoji, kama michuano imefadhiliwa kwa kiasi hicho ni kwa nini wao watozwe fedha nyingi? Na kwa hiyo anasema; "Mashirika ya utangazaji Nigeria tumekataa kulipa Euro milioni nane kwa ajili ya haki ya chombo cha habari kurusha matangazo hayo, tunasikitika kwa Wanigeria kutoweza kuangalia matangazo haya kama walivyotaraji."

No comments:

Post a Comment

Tuachie Ujumbe wako hapa .