Mtayarishaji wa muziki Duke kutoka studio za M Lab ambayo ndio iliwatoa wasanii kama Ben Pol, Grace Matata, Nikki Mbishi, One Incredible na wengine wengi amesema kuwa muziki wa Tanzania umekufa.
Produza alisema hayo wakati akitoa maelezo ya yeye
 kuanzisha 'Kilinge' ambacho huwakutanisha wasanii wa wanaofanya muziki 
wa 'Hip Hop' na kuonyesha uwezo wao kila Jumamosi katika eneo la Msasani
 Club hapa jijini Dar es salaam.
Duke alisema kuwa dhumuni la kuanzisha 'Kilinge' 
ni kuhakikisha kuwa msanii anafanya kitu kwa ufasaha au kwa misingi 
inayotakiwa hii inaamisha kuwa si lazima mtu awe anafanya muziki wa 'Hip
 Hop' ndio afike hapo 'Kilingeni' au Cypher kwa lugha ya kiingereza kama
 watu wanavyodhani.
"Mtu yeyote yule ambaye anafanya muziki 
anaruhisiwa kufika ili tuwekane sawa na tujaribu kuufufua kwa 
kuelekezana". Mimi ni produza na pia kuna watu wengine wanajua kama ni 
muziki wa R&B unatakiwa uimbwe kwa njia zipi.
Hivi karibuni baba yake Dully Sykes alikuja nae 
hapa kushirikiana na sisi kwahiyo hii ni sehemu kwaajili ya kila mtu 
kuja kuonyesha uwezo wake na kuelekezana", Duke.
Alisema kuwa tangu waanzishe utaratibu huo wa 
kukutana kwenye Kilinge kila Jumamosi mpaka sasa ni miezi minne, baadhi 
ya wasanii wakongwe na wanaofanya vizuri waliofika ni Profesa Jay, 
Mapacha, Dan Msimamo, Izzo Biznes na wengine wengi.
Waanzilishi wa Kilinge ni Tamaduni Muziki ambao ni
 kama umoja unaoundwa na Produza Duke na wasanii kama Nikki Mbishi, 
Niite Songa, One Incredible na wengine wengi.


 
 
 
 
 
 
 
 I’m a Freelance Web Designer & Developer. I’m an enthusiastic, creative designer and geek with 3 years of strong commercial experience and a passion for creating beautiful, accessible websites using Web Standards
I’m a Freelance Web Designer & Developer. I’m an enthusiastic, creative designer and geek with 3 years of strong commercial experience and a passion for creating beautiful, accessible websites using Web Standards
No comments:
Post a Comment
Tuachie Ujumbe wako hapa .