![]() |
| Magufuli |
Serikali imesema kwamba itapanua Barabara ya Morogoro kuanzia Dar es Salaam hadi Chalinze.
Akiwasilisha bungeni jana makadirio ya mapato na
matumizi ya wizara yake kwa mwaka wa fedha wa 2013/14, Waziri wa Ujenzi,
Dk John Magufuli alisema lengo ni kupunguza msongamano wa magari na
ajali.
Dk Magufuli alisema upanuzi wa barabara hiyo
utaanzia Dar es Salaam na utakuwa wa umbali wa kilomita 200 na wizara
imetenga kiasi cha Sh100 milioni kwa ajili ya maandalizi.
“Maandalizi ya mradi huo utakaotekelezwa kwa ubia
baina ya Serikali na makampuni binafsi yameanza na makampuni 19
yamewasilisha maombi ya kazi hiyo,” alisema na kuongeza kuwa pia upanuzi
huo utahusu Barabara ya Chalinze-Segera-Tanga yenye urefu wa Kilomita
248.
Alisema utekelezaji wa mradi huo wa pili
umegawanyika katika sehemu mbili ambazo ni Chalinze –Kitumbi (125) na
Kitumbi –Segera –Tanga (km 120). Gharama za ujenzi huo ni Sh3.2 bilioni
zitatokana na fedha za ndani na Sh4.5 bilioni fedha za nje.
Alitaja mradi mwingine mkubwa kuwa ni wa Barabara
ya Kigoma-Kidahwe-Uvinza –Kaliua na Tabora ambayo imetengewa fedha kwa
ajili ya kufanya usanifu na ujenzi wa barabara kwa kiwango cha lami kati
ya Kigoma na Tabora kilometa 443 pamoja na ujenzi wa Daraja la Kikwete
katika Mto Malagarasi.
Dk Magufuli pia alikitaja kipande korofi cha
kuelekea mikoa ya Kusini ya Mtwara na Lindi cha Nangurukuru-Mbwemkulu
chenye urefu wa kilometa 95, akisema kimetengewa Sh2 bilioni.
Alisema pia Wizara ya Ujenzi imetengewa kiasi cha Sh1.2 trilioni kwa mwaka wa fedha wa 2013/14.
Kati ya hizo, fedha za matumizi ya kawaida ni Sh
381.2 milioni na fedha za maendeleo Sh 845.2 bilioni. Alisema kiasi cha
Sh101.3 bilioni kimetengwa kwa ajili ya kujenga barabara kuu zenye jumla
ya urefu wa kilomita 11,276 na madaraja 1,272.
Bilioni moja kwa `fly-over’
Wizara ya Ujenzi imepanga kutumia kiasi cha Sh1
bilioni kwa ajili ya maandalizi ya barabara za kupita juu jijini Dar es
Salaam ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kumaliza tatizo la foleni.


I’m a Freelance Web Designer & Developer. I’m an enthusiastic, creative designer and geek with 3 years of strong commercial experience and a passion for creating beautiful, accessible websites using Web Standards
No comments:
Post a Comment
Tuachie Ujumbe wako hapa .