M-Pesa yapata tuzo ya Superbrand

Wednesday, February 27, 2013



NEMBO ya huduma ya kuweka, kutoa fedha, kununua na kulipia ankara (M-Pesa) kwa bidhaa mbalimbali kupitia simu ya mikononi ya Vodacom ya nchini, imeibuka mshindi kwenye tuzo za ubora wa huduma na viwango za kimataifa za Super Brands kwa mwaka 2013/14.

Akizungumzia tuzo hiyo, Mkurugenzi Mtendaji wa Vodacom, Rene Meza, alisema kuwa ni jambo la kujivunia kwa kampuni yake kufanikiwa kupata tuzo hiyo kubwa na yenye heshima kitaifa na kimataifa.

“Tunawashukuru Watanzania kwa kuendelea kuiunga mkono, kuiamini, kuipokea na kuitumia maradufu huduma ya M-Pesa,” alisema Meza.

No comments:

Post a Comment

Tuachie Ujumbe wako hapa .