Kadi ya Bima ya Afya yazua utata jijini Dar

Monday, January 21, 2013

HOSPITALI ya Hindu Mandal, Dar es Salaam imeuzuia mwili wa Marystela Alfonce aliyefariki juzi baada ya kubainika kuwa alikuwa akitumia kadi ya Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF) ya mtu mwingine aliyetajwa kwa jina la Honorata Magezi ili kupata matibabu. Hospitali hiyo jana ilikataa kutoa mwili wa marehemu Marystela hadi ilipwe Sh7.2 milioni ambazo ni gharama za matibabu tangu alipolazwa hospitalini hapo, Novemba 12, mwaka huu. Mwandishi wetu alishuhudia gari la kubeba maiti aina ya Marcedes Benz lililofika katika chumba cha kuhifadhia maiti cha hospitali hiyo kuchukua mwili wa Marystela likiondoka bila kubeba mwili huo. Ilielezwa kuwa, marehemu alikuwa akitumia kadi ya ndugu yake kupata matibabu katika hospitali hiyo hadi kifo kilipomkuta. kutokana na tukio hilo, mume wa Honorata, Jovis Magezi anashikiliwa na polisi. Magezi ambaye ni Daktari wa Hospitali ya Wilaya ya Mkuranga, alikamatwa jana baada ya kufika Hindu Mandal kwa lengo la kuchukua mwili wa marehemu kabla uongozi wa hospitali hiyo na Bima ya Afya kushtuka. Daktari huyo alikamatwa baada ya maofisa hao kumbana kwa maswali. Mahojiano ya daktari huyo na kikosikazi hicho yalikuwa kama ifuatavyo: Ofisa wa Bima: Mna uhusiano gani na marehemu. Magezi: Ni mke wangu. Ofisa wa Bima: Mke wako alilazwa lini hapa hospitalini? Magezi: Wiki mbili zilizopita.

No comments:

Post a Comment

Tuachie Ujumbe wako hapa .