![]() |
| Mh Nyalandu |
WAJASIRIAMALI nchini, wametakiwa kujenga hoteli za kitalii kwa lengo la kukabiliana na tatizo kubwa la uhaba wa vitanda katika hoteli hizo.
Naibu Waziri wa Maliasilia na Utalii, Lazaro Nyarandu alitoa wito huo mwishoni mwa wiki wakati akizundua hoteli ya kitalii ya Palace ambayo imejengwa kwa ubia na Shirika la Nyumba Nchini(NHC).
Lazaro alisema uwekezaji huo utasadia kuongeza idadi kubwa ya watalii na mapato nchini.
“Mwaka jana tulipata watalii 800,000 ukilinganisha na Rwanda ambayo ilipata 600,000 licha kuwa nchi ndogo, tatizo kubwa la nchi yetu ni upungufu wa vyumba vya kulala wageni,”alisema Nyarandu.
Alisema ujenzi huo utasaidia Mkoa wa Arusha
kuongeza idadi ya vitanda vya kisasa vya kulala wageni. Mkoa wa Arusha
sasa una jumla ya vitanda 2,800 tu, nyuma ya Mkoa wa Dar es salaam
wenye vitanda 3,800 wakati Mkoa wa Mwanza una vitanda 900 licha ya
ukubwa wake.
“Tunaomba shirika la nyumba lijitanue kwa kujenga hoteli za kisasa za kitalii, sisi wizara tunahitaji wawekezaji wa ndani na nje wajitokeze kujenga katika maeneo ya wazi na ndani ya hifadhi zetu, tumejipanga kukabiliana na watumishi wanaokwamisha watu wenye nia njema,”alisisitiza.
“Tunaomba shirika la nyumba lijitanue kwa kujenga hoteli za kisasa za kitalii, sisi wizara tunahitaji wawekezaji wa ndani na nje wajitokeze kujenga katika maeneo ya wazi na ndani ya hifadhi zetu, tumejipanga kukabiliana na watumishi wanaokwamisha watu wenye nia njema,”alisisitiza.
Awali Mkurugenzi Mkuu wa NHC, Nehemia Mchechu
alisema ujenzi wa hoteli hiyo yenye hadhi ya nyota nne, umegharimu Sh16
bilioni na NHC imetoa ardhi na Sh9 bilioni huku kiasi kingine kikitolewa
na Palace Hoteli.
Alisema mradi wa hoteli hiyo ni moja ya miradi
ambayo imekuwa na manufaa makubwa, kutokana na uwazi wa kuendesha hoteli
hiyo na hivyo kuingiza mapato kwa pande zote NHC na mbia.
Naye Dk Macha alisema mradi huo hadi sasa umetoa ajira kwa wafanyakazi 120 na unatoa huduma nyingine kadhaa, ikiwamo huduma za kibenki na utachangia kwa kiasi kikubwa kukuza uchumi wa Mkoa wa Arusha na Taifa.
Naye Dk Macha alisema mradi huo hadi sasa umetoa ajira kwa wafanyakazi 120 na unatoa huduma nyingine kadhaa, ikiwamo huduma za kibenki na utachangia kwa kiasi kikubwa kukuza uchumi wa Mkoa wa Arusha na Taifa.
Akifungua mradi huo rasmi, Waziri wa Nyumba na
Maendeleo ya Makazi, Anna Tibaijuka alipongeza mradi huo na kutoa wito
kwa wajasiriamali kujitokeza na kuingia ubia na NHC katika kutekeleza
miradi mbali mbali.
Alisema mradi huo unakwenda vizuri na umeongeza
mapato ya NHC kwani katika eneo hilo, kabla ya ujenzi wa hoteli walikuwa
wakipata kwa mwaka Sh31 milioni pekee, lakini sasa wanapata Sh151
milioni.


I’m a Freelance Web Designer & Developer. I’m an enthusiastic, creative designer and geek with 3 years of strong commercial experience and a passion for creating beautiful, accessible websites using Web Standards
No comments:
Post a Comment
Tuachie Ujumbe wako hapa .